Kingdom Expansion Series–Swahili

 

Vifaa rahisi, tendaji na vya nguvu vya kupanua Ufalme wa Mungu.

  • Injili Kulingana na Yesu Kristo
  • Kuwafanya Wanafunzi Wafanyao Wanafunzi
  • Kupanda Ushirika wa Nyumbani
  • Kuwafikia ambao hawajafikiwa
  • Kuwahudumia Waislamu

Katika Misururu ya Upanuzi wa Ufalme, utaona maelezo na hadithi za kusisimua, na  mifano ya kawaida, ambayo imeundwa kukusaidia ujifundishe, ufuate, na kupokeza kwa vizazi vijavyo vya wanafunzi. Hizi nyenzo ziliandikwa kusudi ziwe zenye maana na vipengee muhimu pekee. Hizi nyenzo hazina uzito wa kukuchanganyisha. Mafunzo yametengenezwa rahisi ya kujifundisha, kutumia, na kufundisha kizazi kijacho.

Katika kitabu cha kwanza, Injili Kulingana na Yesu Kristo, utawakilishwa na Injili nyororo iliyofundishwa na Yesu na mitume na ikaishi na kanisa la kwanza. Kuwa wa kwanza kujifunza imani ambayo ilibadili kwa ukubwa mno vizazi vya wafuasi wa Kristo, wanaume na wanawake walioupindua ulimwengu juu chini.

Katika kitabu cha pili, Funguo za Upanuzi wa Ufalme, utakusanya habari na mshawasha jinsi wewe binafsi unaweza kuchangia kwa utimilizaji wa Wito Mkuu katika kizazi hiki. Utatiwa changamoto na kuhamazishwa kusalimisha kila kitu kwa Kristo, na kwenda kule inje kuwafanya wanafunzi. Vifaa vya kupitia orodha ya kiroho vimepeanwa kukuongoza wewe kufikia upeo kamili wa uhuru toka dhambini. Ndio, utaona kwamba uhuru toka dhambini ni ukweli wa kimatendo, na sasa unaweza kuufikia.

Kitabu cha tatu, Kanisa Ndani ya Nyumba, kitakuonyesha matendo ya Agano Jipya ya ushirika wa nyumbani. Utajifunza sehemu za kibiblia, utendaji, na kiunabii za kukurejesha kwa urahisi wa matendo ya kanisa yaliyo hai.

Misururu ya Upanuzi wa Ufalme pia ina nyongeza mbili: ya kwanza itakufundisha jinsi ya kupanda ushirika katika maeneo ya watu ambao hawachafikiwa vile Yesu alifanya, jinsi imewakilishwa katika Luka Sura ya 10. Ya pili itakuonyesha jinsi ya kumwakilisha Kristo kwa Waislamu kwa urahisi ukitumia Korani.

 * ALSO AVAILABLE IN ENGLISH AND SPANISH *

 

Kingdom Expansion Series ebook (Swahili)
Get the FREE ebook version of "The Kingdom Expansion Series" in Swahili.
Price: $0.00

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *